Tuesday, 4 August 2015

MANDAGO AWATAKA VIONGOZI KUWA WAVUMILIVU



Gavana wa kaunti ya Uasin Gishu Jackson Mandago, amewataka viongozi wote nchini kuweka tofauti zao za kisiasa kando, ili kuunga mkono sera za serikali kuu iwapo wanataka maendeleo mashinani. Mandago amesema kuwa serikali ya Kaunti ya Uasin Gishu inaunga serikali kuu mkono kwa kila jitihada inazochukua kufanya maendeleo.

Akizungumza na wanahabari afisini mwake  gavana huyo amesema kuwa shida zinazowakumba wakaazi wa kaunti ya Uasin Gishu na Kenya kwa jumla zitakabiliwa tu iwapo viongozi watakuwa tayari kufanya kazi kwa pamoja.

Aidha Mandago amewataka viongozi wote nchini kuwa wavumilivu na kufanya mazungumzo katika kushughulikia shida zinazozikumba serikali za kaunti.