Gavana wa kaunti ya Uasin Gishu Jackson Mandago, amewataka
viongozi wote nchini kuweka tofauti zao za kisiasa kando, ili kuunga mkono sera
za serikali kuu iwapo wanataka maendeleo mashinani. Mandago amesema kuwa serikali ya
Kaunti ya Uasin Gishu inaunga serikali kuu mkono kwa kila jitihada inazochukua
kufanya maendeleo.
Akizungumza na wanahabari afisini mwake gavana huyo amesema kuwa shida zinazowakumba
wakaazi wa kaunti ya Uasin Gishu na Kenya kwa jumla zitakabiliwa tu iwapo
viongozi watakuwa tayari kufanya kazi kwa pamoja.
Aidha Mandago amewataka viongozi wote nchini kuwa
wavumilivu na kufanya mazungumzo katika kushughulikia shida zinazozikumba
serikali za kaunti.