Wednesday, 15 July 2015

KAUNTI YA BUNGOMA - USALAMA WAIMARISHWA KATA NDOGO YA MATULO




     Usalama umeimarishwa katika eneo la Matulo kijiji cha Weighbridge kata ndogo ya Matulo kufuatia visa vya ukosefu wa usalama ambavyo vimekuwa vikishuhudiwa siku za hivi majuzi.

     Mwenyekiti wa mpango wa nyumba kumi katika eneo hilo Thomas Abukuse amesema kuwa, wamekuwa wakitoa taarifa muhimu zinazohusiana na usalama kwa maafisa wa polisi, hatua ambayo imepelekea kuimarika kwa hali ya usalama, huku akitoa wito kwa kwa wadau katika sekta ya usalama kushirikiana zaidi  ili kuwarahisishia majukumu yao.

     Ni mpango ulioanzishwa na serikali ya kitaifa yapata miaka miwili iliyopita, lengo kuu likuwa ni kuimarisha usalama.

No comments:

Post a Comment