Thursday, 16 July 2015

HOSPITALI YA WEBUYE KUKARABATIWA



     Usimamizi wa hospitali ya wilaya ya Webuye utaanzisha shughuli za kurekebisha vyumba vya kuwazalishia akina mama wajawazito hivi karibuni.
     Wakiongozwa na daktari mkuu katika hospitali hiyo Isaac Omeri, viongozi hao wamesema kuwa wana nia ya kuinua sekta ya uzalishaji wa akina mama, ili huduma katika sekta hiyo iimarike zaidi.
     Awali, hospitali ya Webuye ilituzwa kama hospitali bora nchini mwaka wa elfu mbili na kumi na mbili katika huduma za uzalishaji wa akina mama, katika zoezi hilo lililojumuisha hospitali zote za viwango vya nne nchini. Sasa viongozi kwenye hospitali hiyo wanatarajia tuzo zaidi kufuatia ukarabati huo.
     Haya yanajiri huku ukarabati wa vyumba vya kuhifadhi maiti ukiendelea kwenye hospitali hiyo ya Webuye.

No comments:

Post a Comment