Usimamizi wa hospitali ya wilaya ya Webuye utaanzisha
shughuli za kurekebisha vyumba vya kuwazalishia akina mama wajawazito hivi
karibuni.
Wakiongozwa na daktari mkuu katika hospitali hiyo Isaac
Omeri, viongozi hao wamesema kuwa wana nia ya kuinua sekta ya uzalishaji wa
akina mama, ili huduma katika sekta hiyo iimarike zaidi.
Awali, hospitali ya Webuye ilituzwa kama hospitali bora
nchini mwaka wa elfu mbili na kumi na mbili katika huduma za uzalishaji wa
akina mama, katika zoezi hilo lililojumuisha hospitali zote za viwango vya nne
nchini. Sasa viongozi kwenye hospitali hiyo wanatarajia tuzo zaidi kufuatia
ukarabati huo.
Haya yanajiri huku ukarabati wa vyumba vya kuhifadhi
maiti ukiendelea kwenye hospitali hiyo ya Webuye.
No comments:
Post a Comment