Wednesday, 15 July 2015

WEBUYE - DEREVA MAHAKAMANI KUHUSU AJALI YA KIPKAREN



     Dereva wa matatu iliyohusika kwenye ajali ya barabara na kusababisha vifo vya watu tisa eneo la Kipkaren mwezi mmoja uliopita ametozwa faini ya shilingi elfu thelathini pesa taslimu na mahakama ya Webuye.



     Akitoa umamuzi huo hakimu mkaazi wa Webuye Stella Nabwire amesema kuwa mshukiwa huyo kwa jina Vincent Matayo amekiri madai ya kuendesha gari kwa kasi na kukiuka sheria za barabara huku akionywa dhidi ya kurudia kosa hilo na kuwa atapokonywa leseni hiyo ikiwa atahusika kwenye ajali nyingine chini ya miezi sita ijayo.
  
   Nabwire ameitaka mamlaka ya kitaifa ya uchukuzi NTSA kushirikiana na idara ya trafiki kuwahamasisha madereva na wananchi kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria za trafiki ili kupunguza visa vya ajali za barabarani.

No comments:

Post a Comment