Thursday, 16 July 2015

ASANTE LUSAKA - DAKTARI



     Mkuu wa madaktari kwenye hospitali ya wilaya mjini Webuye, amempongeza gavana wa kaunti ya Bungoma Kenneth Lusaka kwa juhudi zake za kuinua viwango vya afya kwenye kaunti hiyo.
     Akizungumza afisini mwake mapema hii leo, daktari Isaac Omeri amesema kuwa serikali ya kaunti imetia fora kuona kuwa afya inapewa kipaumbele, na akamuomba gavana Lusaka kuendeleza juhudi hizo.
     Hata hivyo, Omeri amesema kuwa fedha zinazopeanwa kwa sekta ya afya katika kaunti hiyo ni chache, na kuwa haziwezi kuiendesha sekta hiyo kikamilifu huku akisema kuwa hospitali hiyo imekuwa ikitegemea pesa zinazokusanywa kutoka kwa wagonjwa ambazo pia hazitoshi.
     Vilevile daktari huyo ameomba uongozi wa kaunti hiyo ya Bungoma kutafuta mbinu mbadala za kupata fedha, na kutotegemea serikali ya kitaifa ili kukuza sekta muhimu kwenye kaunti hiyo.

No comments:

Post a Comment